Pogramu ya Innovators-in-Residence 2021-2022
Kituo cha Ubunifu wa Tasnia ya Uanahabari
The Aga Khan University
(Graduate School of Media and Communications)
Kielezo cha Hisia.
Kituo cha AKU GSMC Media Innovation Centre, kwa ushirikiano na DW Akademie, Media Challenge Initiative wanatafuta wabunifu katika tasnia ya uanahabari kutoka Kenya, Uganda na Tanzania watakaojiunga kwenye programu ya Innovators-in-Residence ya mwaka 2021-2022, programu inayoendeshwa kwa kipindi cha miezi 12 ya kukuza na kuchochea ubinifu kupitia ushauri, mafunzo kwa wabunifu katika tasnia ya uanahabari kanda ya Afrika Mashariki.
Lengo letu ni kuhakikisha kwamba wabunifu kutoka maeneo ya vijijini na mjini wanapata fursa ya kujiunga na programu hii na ndio maana, kutakuwa na mpango maalum mahususi kwa ajili ya wabunifu wa kutoka vijijini katika timu itakayoshiriki mwaka huu.
Tunataka kusaidia wabunifu wanaotafuta mbinu za kukuza uanahabari maeneo ya vijijini nchini Tanzania, Uganda na Kenya. Hususan, wabunifu wenye miradi inayowafikishia wananchi habari, kuhimiza mijadala ya wazi sambamba na kuimarisha kushirikishwa kwa jamii za vijijini ikizingatiwa changamoto za uwepo wa lugha mbalimbali, upatikanaji mdogo wa mtandao wa intaneti, upatikanaji mdogo wa habari kutoka kwa vyombo vikubwa vya habari na viwango vya chini vya elimu. Wabunifu wanaoendesha shughuli zao nje ya miji kama Nairobi, Dar es Salaam na Kampala wanahimizwa sana kutuma maombi.